Tupashane Habari 24-hours

Tupashane Habari 24-hours

Breaking News

kampa kampa tena

HAWATOKI WATAKE WASITAKE.

Ushindi wa idadi yoyote ya mabao katika mchezo wa kesho dhidi ya Mbeya City utakaochezwa Uwanja wa Sokoine, Mbeya utaipa ubingwa Azam kwani itafikisha pointi 59 ambazo haziwezi kufikiwa na timu yoyote katika ligi hiyo.

HAWATOKI. Ligi Kuu Bara imefikia patamu huku Azam FC na Yanga zikipigana kufa na kupona kutwaa ubingwa, lakini mechi iliyobeba gumzo ni ile itakayochezwa Jumapili (kesho) kati ya Mbeya City na Azam huku kila upande ukikataa kupoteza mchezo huo.
Azam chini ya Kocha, Joseph Omog ipo kileleni katika msimamo wa ligi hiyo ikiwa na pointi 56 ikifuatiwa na Yanga yenye pointi 52 na Mbeya City ni ya tatu ikiwa na pointi 46. Timu zote zimecheza mechi 24 na kubakiwa na michezo miwili.
Ushindi wa idadi yoyote ya mabao katika mchezo wa kesho dhidi ya Mbeya City utakaochezwa Uwanja wa Sokoine, Mbeya utaipa ubingwa Azam kwani itafikisha pointi 59 ambazo haziwezi kufikiwa na timu yoyote katika ligi hiyo. Yanga ikishinda mechi zake mbili itafikisha pointi 58 tu.


VITA YA UBINGWA
Mechi mbili za kesho Jumapili kati ya Mbeya City na Azam na JKT Oljoro na Yanga zitatoa picha ya ubingwa msimu huu lakini, macho ya mashabiki wengi yatakuwa Mbeya katika mechi ya Azam na Mbeya City.
Katika mchezo wa kwanza Novemba mwaka jana kwenye Uwanja wa Chamazi, Mbagala Dar es Salaam, timu hizo zilitoka sare ya mabao 3-3 huku zote zikiweka rekodi ya kutofungwa mchezo wowote katika mzunguko huo.
Akizungumzia mchezo huo, Kocha wa Azam, Omog alisema: “Kila mechi ni ngumu kwetu, lakini tutahakikisha tunashinda mechi yetu ya Mbeya City na kutangaza ubingwa.
“Tumekuwa na malengo ya ubingwa kwa muda mrefu na Jumapili ndiyo siku yetu, tutapigana kwa nguvu zote ili tushinde.”
Lakini Kocha Msaidizi wa Azam, Kally Ongalla alisema: “Mbeya City wana mashabiki wengi lakini wakumbuke kuwa tumezifunga Simba na Yanga zenye mashabiki wengi kuliko timu zote za soka hapa nchini.”
Beki wa kati wa Azam, Aggrey Morris alisema: “Tuna kila sababu ya kuifunga Mbeya City na kutangaza ubingwa wetu, hatuwezi kufanya mchezo juu ya hilo.”
Kocha wa Mbeya City, Juma Mwambusi alisema: “Mashabiki waje kwa wingi kuona mechi nzuri na ya ushindani, tumejipanga kuicheleweshea Azam ubingwa. Hatutakubali kufungwa nyumbani kwetu.”
Katibu Mkuu wa Mbeya City, Emmanuel Kimbe amelalamikia proganda nyingi chafu zinazozushwa na baadhi ya watu katika kuelekea mchezo huo ambazo siyo sahihi.

No comments