Tupashane Habari 24-hours

Tupashane Habari 24-hours

Breaking News

kampa kampa tena

Ngoma atinga anga za Mahrez, Chicharito Na whezron - May 17, 2016 250 0


NA MWANDISHI WETU
DONALD Ngoma kesho atashuka kwenye Uwanja wa Nelson Mandela kuitumikia timu yake ya Yanga itakayokuwa ikipepetana na G.D Sagrada Esperanca ya Angola, huku akiwa amefanikiwa kufanya kile kilichofanywa na wakali wa mabao Ulaya kama Riyad Mahrez wa Leicester City ya England, Javier Hernandez ‘Chicharito’ wa Leverkusen ya Ujerumani, Boria Gonzalez wa Eibar ya Hispania, Carlos Bacca wa AC Milan ya Italia, Lucas Martinez wa Deportivo La Coruna ya Hispania na wengineo.
Hadi sasa Yanga ikiwa imecheza mechi 29 za Ligi Kuu Tanzania Bara, Ngoma ameshafunga mabao 17 msimu huu kama ilivyo kwa wakali hao katika ligi wanazocheza.
Wakati ligi za Ulaya zikiwa zimeshafikia ukingoni, kule England, Harry Kane wa Tottenham ndiye aliyeibuka kinara wa mabao kwa kucheka na nyavu mara 25, huku Hispania mbabe wao akiwa na Luis Suarez wa Barcelona mwenye mabao 40.
Huko Ujerumani, aliyefunga mabao mengi zaidi ni  Robert Lewandowski wa Bayern Munich (30), Italia ni Gonzalo Higuin wa Napoli (36) na Ufaransa ni Zlatan Ibrahimovic wa Paris Saint-Germain (PSG) aliyetikisa nyavu mara 38.
Hata hivyo, Ngoma anaweza kuongeza idadi ya mabao ya kufunga wakati Yanga itakapoivaa Majimaji katika mchezo wao wa mwisho wa ligi Jumapili hii kwenye Uwanja wa Majimaji, Songea.
Wakati hali ikiwa hivyo kwa Ngoma, pacha wake katika safu ya ushambuliaji ya Yanga, Amissi Tambwe, hadi sasa amefunga mabao 21 ambapo iwapo atatikisa nyavu zaidi ya mara tatu Jumapili dhidi ya Majimaji, anaweza kufikia idadi ya mabao yaliyofungwa na
washambuliaji tishio Ulaya kama Jamie Vardy wa Leicester City mwenye 24, Edinson Cavani wa PSG (21), Lionel Messi wa Barcelona (26), Karim Benzema wa Real Madrid (24), Neymar wa Barecona (24), Antoine Griezmann wa Atletico Madrid (22), Pierre-Emerick Aubameyang wa Borussia Dortmund na wengineo.
Ngoma na Tambwe wametoa mchango mkubwa katika kikosi cha Yanga na hatimaye kutwaa ubingwa wa Bara wakiwa na mechi tatu mkononi.
Mchezo wa Jumapili utakuwa wa mwisho kufunga msimu huu na hivyo kujiandaa na msimu ujao kutetea ubingwa wao kwa mara nyingine.

Source: http://bingwa.co.tz/wp-content/uploads/2015/09/BingwaLogo1.png

No comments