Maamuzi ya Kamati ya Maudhui juu ya Radio 5 Kukiuka Kanuni za Utangazaji:
Kituo kilivunja Kanuni za Maudhui kwa Kumkashifu Rais na Serikali na
kuchochea na kuhamasisha uvunjifu wa amani, kupambana na Polisi.
Maamuzi:
1. Fine shilingi 5 million
2. Kufungiwa kwa miezi 3
3. Inawekwa chini ya uangalizi kwa mwaka mmoja.
Magic FM yafunguliwa
Kamati ya maudhui ya Mamlaka ya mawasiliano Tanzania imekifungulia rasmi kituo cha radio cha Magic Fm cha jijini Dar es salaam
Radio Magic fm ilifungiwa kwa muda usiojulikana na Waziri Nape Nauye
Agosti 29, 2016 kwa tuhuma za kutangaza kipindi kinachodaiwa kukiuka
sheria za utangazaji
Kwa mujibu wa David Ramadhan aliyekuwepo wakati wa kusoma maamuzi ya
kamati ya maudhui ya Mamlaka ya mawasiliano Tanzania, kamati hiyo
imeitaka Radio Magic fm kutekeleza yafuatayo..
1)Kutoa onyo kali radio Magic Fm
2)Kuomba radhi kwa Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania, John
Magufuli na wasikilizaji wake, hivyo inatakiwa kuomba radhi kwenye
taarifa za habari na tangazo lipewe nafasi kubwa.
Maamuzi hayo yamesomwa na makamu Mwenyekiti wa kamati ya maudhui Joseph Mapunda.
SOURCE: JAMIIFORUMS
TCRA yaifungia Radio 5 miezi 3 pamoja na faini, Magic Fm yafunguliwa kwa masharti
Reviewed by
Unknown
on
7:48 AM
Rating:
5
No comments