Tupashane Habari 24-hours

Tupashane Habari 24-hours

Breaking News

kampa kampa tena

Sema Ghana wametisha sana na hii kampuni inayotengeneza magari.. ( picha 14 )

Pamoja na hizi picha zaidi ya kumi kwenye hii post, inabidi ufahamu haya mambo matatu ya hii kampuni ya raia wa Ghana ambayo imeanza kupata mapokezi mazuri kwenye biashara ambayo ni mpya kwenye bara la Afrika, nchi ya Afrika inayounda magari.
Kampuni inaitwa Kantanka Group na mpaka sasa wanaweza kutengeneza magari mapya mia moja kila mwezi… pia gari la bei rahisi zaidi linagharimu MILIONI 40 za Kitanzania.
cnn 10
Mafundi wakiwa kwenye moja ya hatua za kuunda gari
Katika changamoto wanazokutana nazo ni kwamba baadhi ya watu hawana imani yani kuona gari limetengenezwa Afrika na Waafrika, wengine wanahoji halichomoki mlango likiwa spidi? sio bovubovu? C.E.O Kwadwo Safo Jr. anasema kwa miezi sita waliwapa Polisi wa Ghana magari ya kujaribu na mpaka leo hawajapata lalamiko lolote.
cnn 13
Zamani watoto wa kiafrika walikua wakionekana kuunda magari yao ya mbao lakini ukiyatazama unaona kabisa akili iliyotumika hapa sio ya kawaida, wengine walijaribu hata kuunda ndege na Helikopta Kenya na Nigeria ila sasa ndoto zimeanza kutimizwa….. naamini hii itawapa wengine nguvu ya kujiamini na kujaribu.
cnn 8
cnn 5
cnn 7
Hii ni moja ya aina ya magari yaliyotengenezwa na kampuni hii ya Ghana.
cnn 2
cnn 4
cnn 3
cnn 1
cnn 6
cnn 11
Magari yenyewe wanayoyatengeneza
cnn 12
cnn 14
Picha zote ni kutoka CNN.

No comments