Ripoti kutoka Mahakama ya Rufaa Dar es Salaam kwenye Kesi ya Mawaziri wa zamani, Basil Mramba na Daniel Yona..
July 06 2015
ilisambazwa Taarifa kwenye Vyombo vya Habari kuhusu Mahakama ya Kisutu
Dar es Salaam kutoa hukumu ya kifungo cha miaka mitatu jela kila mmoja
kwa Mawaziri wa zamani, Basil Pesambili Mramba, na Daniel Yona baada ya kukutwa na hatia ya Kesi ya kuisababishia hasara Serikali pamoja na matumizi mabaya ya madaraka.
Mbali na hukumu ya kifungo cha miaka miwili jela, Mramba na Yona walitakiwa pia kulipa faini ya Milioni tano kila mmoja.
Ninayo Ripoti nyingine kutoka Mahakama ya Rufaa Dar es Salaam… Rufaa ya Kesi hiyo imefikishwa kwenye meza ya Mahakama ya Rufaa na Mahakama hiyo imeikataa Rufaa hiyo.
Kingine kilichoamriwa ni kwamba
watuhumiwa wote wawili wamepunguziwa adhabu ya kifungo, kwa sasa
watatumikia miaka miwili jela na adhabu ya faini imeondolewa.
Source: Millard Ayo
No comments