Tupashane Habari 24-hours

Tupashane Habari 24-hours

Breaking News

kampa kampa tena

Pale ambapo Refa anaamua kutumia Bastola baada ya mambo kuharibika Uwanjani..

Mara nyingi tumezoea kuona waamuzi wakitumia madaraka yao kuwaonya wachezaji soka uwanjani kwa kadi za manjano na kadi nyekundu kama kosa ni kubwa, lakini hii imekuwa tofauti kidogo kwa muamuzi Gabriel Murta ambaye alitumia zaidi ya kadi na filimbi kujihami uwanjani.
Gabriel Murta alipatwa na hasira uwanjani na inadaiwa alienda katika vyumba vya kubadilishia nguo na kurudi na bastola uwanjani huku akimuonyeshea moja kati ya wachezaji waliokuwa wakicheza mechi hiyo, tukio hilo lilitokea katika Ligi za madaraja ya chini Brazil, kwani ilikuwa ni mechi kati ya Brumadinho dhidi ya Amantes da Bola.
refereemain1_3456783b
Video ya tukio hilo ilirekodiwa na moja kati ya mashabiki waliokuwa wamehudhuria mchezo huo, stori kutoka kwa watu waliokuwemo katika mchezo huo ni kuwa, tukio hilo lilitokea baada ya viongozi wa klabu ya  Amantes da Bola kuvamia uwanja na kumshinikiza Murta kutoa kadi nyekundu kwa mchezaji wa timu pinzani.
295012
Meneja wa chama cha waamuzi Giuliano Bozzano amenukuliwa akisema kuwa muamuzi huyo alitoa bastola uwanjani ili kujihami mwenyewe, kwani kulikuwa na uwezekano wa kufanyiwa vurugu na wachezaji na viongozi wa klabu ya Amantes da Bola waliokuwa wameingia uwanjani. kufuatia tukio hilo Gabriel Murta ambaye alikuwa muamuzi wa mechi hiyo, huenda akafungiwa kujihusisha na soka kwa muda mrefu au maisha



Source: Millard Ayo

No comments