Tupashane Habari 24-hours

Tupashane Habari 24-hours

Breaking News

kampa kampa tena

KOMBE LA DUNIA: GERMANY, NIGERIA ZATANGAZA VIKOSI VYA AWALI!

GERMANY: MERTESACKER, PODOLSKI, OZIL WA ARSENAL NDANI, MARIO GOMEZ NJE!
NIGERIA: YOBO, ODEMWINGIE WAREJESHWA KUNDINI!

BAADA WENYEJI wa Fainali za Kombe la Dunia zitakazochezwa kuanzia Juni 12, Brazil, kutangaza Kikosi chao cha awali, Nchi za Germany na Nigeria nao wametangaza Vikosi vyao vya awali vya Wachezaji 30 kila mmoja.
GERMANY
Wachezaji watatu wa Arsenal, Per Mertesacker, Lukas Podolski na Mesut Ozil, ni miongoni mwa Wachezaji 30 waliotangazwa na Kocha, Joachim Low, kwenye Kikosi cha awali cha Germany kwa ajili ya Fainali za Kombe la Dunia.
Mchezaji mwingine pekee toka Ligi Kuu England ni Andre Schurrle wa Chelsea.
Nae Kiungo wa Real Madrid Sami Khedira ametajwa licha ya kutocheza tangu Novemba alipoumia vibaya Goti lakini Straika wa Fiorentina, Mario Gomez, ambae nae aliumia na kuwa nje kwa Miezi 7 na tangu arejee Mwezi Septemba amekuwa akicheza kwa nadra, hayumo kwenye Kikosi hicho.
Kwenye Kikosi hicho, Bayern Munich imetoa Wachezaji 7 na Dortmund Dortmund 6.
Kila Nchi inayocheza Fainali inatakiwa ipeleke Majina ya Wachezaji wao wasiozidi 30 kwa FIFA ifikapo Mei 13 na Listi ya mwisho ya Wachezaji 23 inatakiwa iwasilishwe Juni 2.
KIKOSI KAMILI:
MAKIPA: Neuer (Bayern Munich), Weidenfeller (Dortmund), Zieler (Hanover)
MABEKI: Boateng (Bayern Munich), Durm (Dortmund), Grosskreutz (Dortmund), Hoewedes (Schalke), Hummels (Dortmund), Jansen (Hamburg), Lahm (Bayern Munich), Mertesacker (Arsenal), Mustafi (Sampdoria), Schmelzer (Dortmund).
VIUNGO: Bender (Leverkusen), Draxler (Schalke), Ginter (Friburg), Goretzka (Schalke), Goetze (Bayern Munich), Hahn (Augsburg), Khedira (Real Madrid), Kroos (Bayern Munich), Meyer (Schalke), Muller (Bayern Munich), Ozil (Arsenal), Podolski (Arsenal), Reus (Dortmund), Schurrle (Chelsea), Schweinsteiger (Bayern Munich)
MAFOWADI: Klose (Lazio), Volland (Hoffenheim)
NIGERIA
Nigeria imewarejesha tena Kikosini Joseph Yobo na Peter Odemwingie katika Kikosi chao cha awali cha Wachezaji 30 cha Fainali za Kombe la Dunia.
Mara ya mwisho kwa Yobo kuichezea Nigeria ni Mwaka Jana kwenye Fainali za AFCON huko Afrika Kusini wakati Odemwingie, anaechezea Stoke City, amekuwa akiachwa na Kocha Stephen Keshi baada kugomba nae tangu kabla ya AFCON 2013.
Wachezaji maarufu ambao wameachwa ni pamoja na Brown Ideye na Fegor Ogude wanaocheza Klabu za Ukraine.
KIKOSI KAMILI:
MAKIPA: Vincent Enyeama (Lille/France), Austin Ejide (Hapoel Be'er Sheva/Israel), Chigozie Agbim (Gombe United, Nigeria), Daniel Akpeyi (Warri Wolves, Nigeria)
MABEKI: Elderson Echiejile (Monaco/France), Efe Ambrose (Celtic FC/Scotland), Godfrey Oboabona (Rizespor/Turkey), Azubuike Egwuekwe (Warri Wolves, Nigeria), Kenneth Omeruo (Middlesbrough/England), Juwon Oshaniwa (Ashdod FC/Israel), Joseph Yobo (Norwich City/England), Kunle Odunlami (Sunshine Stars, Nigeria)
VIUNGO: Mikel Obi (Chelsea/England), Ogenyi Onazi (SS Lazio/Italy), Ramon Azeez (Almeria/Spain), Ejike Uzoenyi (Enugu Rangers, Nigeria), Gabriel Reuben (Beveren/Belgium), Nosa Igiebor (Real Betis/Spain), Joel Obi (Parma/Italy), Michael Uchebo (Cercle Brugge/Belgium), Sunday Mba (CA Bastia/France)
MAFOWADI: Ahmed Musa (CSKA Moscow/Russia), Shola Ameobi (Newcastle United/England), Victor Moses (Liverpool/England), Emmanuel Emenike (Fenerbahce/Turkey), Obinna Nsofor (Chievo Verona/Italy), Peter Osaze Odemwingie (Stoke City/England), Babatunde Michael (Volyn/Ukraine), Nnamdi Oduamadi (Varese/Italy), Uche Nwofor (Heerenveen/Netherlands)

No comments