Tupashane Habari 24-hours

Tupashane Habari 24-hours

Breaking News

kampa kampa tena

Chelsea inakaribia kumsajili staa huyu, wakati ambao Pedro anaanza safari ya kurudi Barcelona …

Stori kutoka katika mitandao mbalimbali barani Ulaya hususani Uingereza, imekuwa ikiripoti kwa karibu mpango wa Chelsea kutaka kusajili nyota wapya kikosi. Chelsea siku kadhaa nyuma ilikataliwa kumsajili kiungo wa Shakhtar Donetsk Alex Teixeira licha ya kutoa ofa ya pound milioni 30.
January 21 stori kutoka express.co.uk inaripoti kuwa klabu ya Chelsea ipo katika hatua za mwisho kukamilisha mazungumzo ya kumsajili Alexandre Pato kutoka klabu ya Corinthians, lakini kama itashindikana wataomba kumchukua kwa mkopo. Chelsea pia inahusishwa kutaka kumsajili Carlos Bacca wa AC Milan na Saido Berahino wa West Brom.
Alexandre-pato-636517
Stori za usajili za Chelsea hazijaishia kwa upande wa kusajili pekee, bali wanatajwa kuwa na mpango wa kumuuza Pedro Rodriguez mwishoni mwa msimu kurudi katika klabu yake ya zamani ya FC Barcelona. Pedro ambaye amesajiliwa dakika za mwishoni za usajili wa dirisha la majira ya joto.

No comments