Usisahu kuwa Yanga imecheza leo dhidi ya JKT Mlale FA Cup, matokeo haya
Jumatano ya February 23 klabu ya Dar Es
Salaam Young African ilikuwa mwenyeji wa klabu ya JKT Mlale katika
mchezo wao wa hatua ya 16 bora yaa Kombe la FA ambalo linafahamika kama
Azam Sports Federation Cup (ASFC), Yanga walishuka uwanja wa Taifa
wakiwa wamebadili kikosi chao tofauti na kilivyozoeleka.
Kikosi cha Yanga ambacho kilisaidia
kuibuka na ushindi wa goli 2-1 dhidi ya JKT Mlale, kiliamua kuwaanzisha
wachezaji kama Matheo Anthony na Geofrey Mwashiuya na Said Juma, kwa
kile ambacho kinaaminika ni kuwapumzisha wachezaji wa kikosi cha kwanza
kwa ajili ya mechi ya klabu Bingwa Afrika dhidi ya klabu ya Cercle de
Joachim ya Mauritius.
Yanga walianza kwa kuruhusu goli, baada
ya Shabani Mgandila kutumia vyema makosa ya safu ya ulinzi na kupatia
goli la kwanza dakika ya 22, licha ya kuwa Yanga walikuwa wanajiamini na
kucheza kwa dharau, walifanikiwa kusawazisha goli dakika ya 38 kupitia
kwa Paul Nomga na dakika ya 58 Thabani Kamusoko akapachika goli la pili
na la mwisho kwa Yanga baada ya kutumia vyema pasi ya Geofrey Mwashiuya.
Source: Millard Ayo.
No comments